1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

FBI wahudhuria kesi ya Sudan Kusini

Saumu Mwasimba
6 Juni 2017

Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI) linahudhuria siku ya pili ya kusikilizwa kesi dhidi ya wanajeshi wanaotuhumiwa katika mashambulizi mabaya kabisa dhidi ya wafanyakazi wa kigeni nchini Sudan Kusini.

https://p.dw.com/p/2eBDq
Südsudan Kinder
Picha: picture-alliance/NurPhoto/M. Moskwa

Wanaume 12 wanatuhumiwa kwa ubakaji, mateso na mauaji katika shambulio la mwezi Julai katika hoteli ya Terrain ilioko katika mji mkuu wa Sudan Kusini Juba.

Marekani imetoa msaada kwa ajili ya uchunguzi huo na msemaji wa ubalozi wa Marekani amesema uwepo wa FBI nchini Sudan Kusini umetokana na majadiliano.

Serikali ya Sudan Kusini inasema Marekani imetoa msada wa kiufundi na kiuchunguzi kuwabaini watuhumiwa.

Mahakama leo imekataa ombi la upande wa mashitaka la mapunmziko ya mwezi mmoja ili kujiandaa zaidi.

Wengi wa waathirika wa kisa hicho wanaishi nje ya nchi.