Wafanyabiashara wakubwa wanazidi kuiamini mitandao ya kijamii na vijana wameanza kuwekeza kwenye kusaka matangazo ya kampuni kubwa kubwa kupitia mitandao hiyo. Meneja Mkurugenzi wa Kampuni ya Jamii Media ya Dar es Salaam, Tanzania, Maxence Mello, inayoendesha mtandao wa Jamii Forum unaoongoza kwa kuwa na wasomaji wengi barani Afrika, anazungumzia fursa za kibiashara kupitia mitandao ya kijamii.