1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BERLIN: Merkel kuzuru Mashariki ya Kati

30 Machi 2007
https://p.dw.com/p/CCE3

Kansela wa Ujerumani Bi Angela Merkel ataondoka kesho kuanza ziara yake ya siku tatu ya Mashariki ya Kati. Ziara yake itajumulisha mazungumzo na rais wa mamlaka ya Palestina, Mahmoud Abbas, mjini Ramallah. Bi Merkel atakutana pia na waziri mkuu wa Israel, Ehud Olmert mjini Jerusalem.

Ziara hiyo inafanyika kufuatia mkutano wa viongozi wa kiarabu mjini Riyadh, Saudi Arabia, ambapo mpango mpya wa amani ya Mashariki ya Kati ulifufuliwa. Mkutano huo uliitaka Israel iukabali mpango huo.