BERLIN: Abbas akutana na Merkel
23 Februari 2007Matangazo
Rais wa mamlaka ya Palestina Mahmoud Abbas anakutana na kansela wa Ujerumani Bi Angela Merkel mjini Berlin hapa Ujerumani.
Baada ya kukutana hapo awali na waziri wa mashauri ya kigeni wa Ujerumani, Frank Walter Steinmeier, rais Abbas ametoa mwito mgomo dhidi ya serikali ya Palestina kufuatia ushindi wa kundi la Hamas kwenye uchaguzi wa bunge, umalizike.
Waziri Steinmeier alisisitiza sharti la pande nne zinazoudhamini mpango wa amani ya Mashariki ya Kati kwamba serikali mpya ya Palestina itatakikwa ilaani machafuko na iitambue haki ya kuwepo kwa taifa la Israel.