1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Benazir Bhutto hatotishwa na mashambulizi

P.Martin20 Oktoba 2007

Waziri Mkuu wa zamani wa Pakistan,Benazir Bhutto atagombea uchaguzi mkuu ujao,licha ya shambulizi la siku ya Alkhamisi mjini Karachi.

https://p.dw.com/p/C77e
Benazir Bhutto akizungumza na waabdishi wa habari nyumbani kwake mjini Karachi
Benazir Bhutto akizungumza na waabdishi wa habari nyumbani kwake mjini KarachiPicha: AP

Bhutto amesema,shambulizi hilo ni dhidi ya demokrasia, umoja na uadilifu wa Pakistan.

Mshambulizi aliejitolea maisha muhanga,alijiripua kati kati ya umati uliokuwa ukimkaribisha Bhutto kwa shangwe kubwa,aliporejea Pakistan baada ya kuishi uhamishoni kwa miaka minane iliyopita. Zaidi ya watu 130 waliuawa na kama 250 wengine wamejeruhiwa.Bhutto binafsi hakuumia.

Wanamgambo wenye itikadi kali za kiislamu wamelaumiwa na serikali kuhusika na shambulizi hilo ambalo ni baya kabisa kupata kufanywa nchini Pakistan.