1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Balaa linalosababishwa na mafuta yanaomwagika baharini

Oumilkher Hamidou22 Juni 2010

Madhara ya maszingira na mimea pamoja na viumbe vya baharini katika ghuba ya Mexico yanatishia kulingana na yale yaliyotokea miaka 21 iliyopita Alaska

https://p.dw.com/p/NzwG
Mafuta yanayochafua Ghuba ya MexicoPicha: AP

Michelle Ridgway ni mtaalam wa elimu ya viumbe wa baharini na kawaida anakua akisomea mfumo wa ekolojia katika eneo la Alaska.Uchunguzi anaofanya ndio unaomuwezesha kutambua kwa jinsi gani mabadiliko ya hali ya hewa yanashawishi pia ukuaji wa viumbe tofauti vya baharini. Mtaalam huyo wa kimarekani anatafutwa sana hivi sasa ili aseme kama anaweza kupiga mbizi katika ghuba ya Mexico na kufanya uchunguzi.Mtaalam huyo ameshawahi kutoa maelezo na data chungu nzima kuhusu maisha ya viumbe vya baharini na kitisho wanachokumbana nacho-tangu meli ya mafuta ya Exxon Valdez ilipovuja mwishoni mwa miaka ya 80 katika eneo la Prince-William Sund.

Kwa zaidi ya miaka 20 sasa Michelle Ridgway amekua akitumia mashua ndogo inayokwenda chini ya bahari katika eneo la Bering See huko Alaska.Mtaalam huyo wa biolojia ya viumbe vya baharini huingia ndani ya chombo kidogo na kupiga mbizi kina cha mita 100 chini ya bahari na kufanya uchunguzi wake.Hufanya hivyo anapotaka kukusanya maelezo kuhusu kwa mfano athari zinazosababishwa na mabadiliko ya hali ya hewa baharini.

"Kuna mabadiliko ya hali ya hewa,hali hiyo inaonekana katika tabaka za juu za uso wa bahari kwa kuangalia jinsi mimea na viumbe vya baharini vinavyobadilika maji ya bahari yanapokua na ujoto.Na katika tabaka za chini kabisa za bahari kwenye hali ya ujoto, tunaona papa wengi,aina tofauti za papa katika Bering See."

Flash-Galerie Ölpest Eindämmung
Meli inayojaribnu kuzuwia mafuta yasichafuwe fukwe za bahariPicha: AP

Michelle anakuja na picha za kusisimua anazopiga katika maeneo hayo ya chini ya bahari na kuchapishwa pia katika jarida la National Geographic Magazine.Hivi sasa mtaalam huyo anaombwa akapige mbizi pia katika Ghuba ya Mexico.Kwasababu miaka 21 iliyopita alikua wa mwanzo kufanya utafiti katika kina cha bahari meli ya mafuta ya Exxon Valdez ilipomwaga mafuta na kuchafua mazingira huko Prince William Sund katika eneo la Alaska.

Michelle Ridgway anasema:

"Wakati ule tangu idadi mpaka aina za mimea na viumbe vya baharini viliathirika.Na tunaamini hali kama hiyo inaweza pia kutokea katika Ghuba ya Mexico.Tunaelewa hofu na wasi wasi wa wakaazi wa eneo la Ghuba ya Mexico.Kile watakachojionea ni kuvurugika mfumo wa ekolojia kwa kipindi cha zaidi ya miaka kumi ijayo."

Hali kama hiyo imetokea pia Alaska.

"Maafa yana madhara ya muda mrefu,lakini katika mfumo wa ekolojia kuna baadhi ya viumbe na mimea ambayo ni sugu.Balaa lililosababishwa na mafuta yaliyomwagika limeathiri aina mbali mbali za mimea na viumbe ,lakini kwa daraja tofauti.Kuna aina fulani ya samaki wajulikanao kama heringi wameathirika vibaya zaidi.Samaki hao hawakurejea tena na hali kama hiyo inaisibu mimea na viumbe vyengine kadhaa."

Michelle Ridgway amefungua tovuti yake mwenyewe ambapo anakua anachapisha ripoti kuhusu utafiti anaofanya.Watu wengi wanapenda kufuatuilizia yaliyoandikwa na mtaalam huyo.

Mwandishi: Tussing Jan /ZR/Hamidou,Oummilkheir

Imepitiwa na::Abdul-Rahman,Mohammed