1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Baa la njaa na ukame lasababisha wimbi la wakimbizi nchini Kenya

11 Julai 2011

Hali mbaya ya ukame iliyozikumba nchi za eneo la Pembe ya Afrika, pamoja pia na eneo la Kaskazini mwa Kenya, imesababisha maelfu ya watu kuzikimbia nyumba zao na kwenda kutafuta hifadhi katika makambi ya wakimbizi.

https://p.dw.com/p/11t91
Wanawake na watoto wa Kisomali wakiwa katika foleni ya kupata chakulaPicha: dapd

Hali mbaya ya ukame iliyozikumba nchi za eneo la Pembe ya Afrika Ethiopia Djibouti na Somalia, pamoja pia na eneo la Kaskazini mwa Kenya imesababisha maelfu ya watu kuzikimbia nyumba zao kila siku na kwenda kutafuta hifadhi katika makambi ya wakimbizi, ambako wanaweza kupata msaada wa chakula.

Kambi ya wakimbizi ya Dadaab nchini Kenya kwa sasa  imekuwa ikipokea wakimbizi hao wanaokimbia makaazi yao kutokana na Ukame na njaa hasa kutoka nchini Somalia.