Aliandika, akafungwa, akaadhibiwa, akaandika tena na tena
Mohammed Khelef23 Julai 2015
Wengi wanamtambua kwa kazi yake ya Sauti ya Dhiki, diwani ya mashairi ya miaka ya '80, lakini si wengi wanaojuwa kuwa Abdilatif Abdulla ni mwanasiasa mkongwe wa Kenya ambaye amekuwa mwanaharakati wa mageuzi tangu ujana wake. Katika dakika hizi 60 na DW, mwanafasihi na mshairi huyu mashuhuri anasimulia hadithi ya maisha yake.