1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

ABUJA:Mgomo Nigeria

20 Juni 2007
https://p.dw.com/p/CBq6

Mgomo wa Wafanyikazi umeanza nchini Nigeria.

Mgomo huo ambao haujulikani utamalizika lini huenda ukalemaza shughuli nyingi katika taifa hilo la Africa linalotoa kiasi kikubwa cha mafuta.

Vyama vya wafanyikazi vimekataa mapendekezo ya serikali ya kutaka kufikiwa makubaliano vikisema ni hatua iliyokuja kuchelewa.

Vyama hivyo vimewataka wafanyikazi wa Benki,shule na masoko nchini humo kushiriki mgomo huo.

Wafanyikazi wanapinga kima cha chini cha mishahara, kiasi kikubwa cha kodi ,kupanda kwa bei ya mafuta ya petroli pamoja na ubinafisishaji wa kampuni mbili za mafuta.

Serikali hapo jana ilisema itaongeza mshahara kwa asilimia 15 na kupunguza kodi ya ongezeko la thamani kutoka asilimia 10 hadi asilimia tano.