ABUJA: Mfanya maandamano apigwa risasi na polisi
14 Oktoba 2006Matangazo
Polisi nchini Nigeria wamempiga risasi na kumuua mwaandamanaji mmoja katika maandamano yaliofanywa Jos,mji mkuu wa jimbo la Plateau.Polisi walifyatua risasi kuutawanya umati uliokuwa ukipinga hatua ya kutaka kumshtaki gavana wa jimbo hilo kutumia vibaya madaraka.Mashahidi wamesema,waandamanaji hao baadae walikusanyika upya na wakalitia moto jengo moja.