Jana usiku afisa mmoja wa polisi aliuliwa na wengine wawili kujeruhiwa na mtu mmoja aliyewashambulia kwa risasi katika mji mkuu Paris, Ufaransa// Polisi ya Ujerumani imemtia mbaroni mwanamme Mjerumani mwenye asili ya Urusi, anayeshukiwa kufanya mashambulizi dhidi ya basi lililokuwa likiwasafirisha wachezaji wa klabu ya Borussia Dortmund wiki iliyopita.