Kansela Angela Merkel amejibu lawama za rais mteule wa Marekani Donald Trump dhidi ya siasa yake ya kiliberali kuelekea wakimbizi na tuhuma zake dhidi ya jumuiya ya kujihami ya NATO// Waziri mkuu wa Uingereza Theresa May leo anatarajiwa kuelezea kwamba anaunga mkono utaratibu safi wa kujitoa kutoka Umoja wa Ulaya, na kuondoa uwezekano wa kujiondoa kwa sehemu tu katika mikataba na Umoja huo.