1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

11 wauwawa Mogadishu

24 Machi 2007
https://p.dw.com/p/CCFo

MOGADISHU:

Watu 11 wameuwawa nchini Somalia baada ya ndege iliotunguliwa kuanguka wakati ikiruka kutoka uwanja wa ndege wa Mogadishu.

Waziri wa mambo ya ndani wa serikali ya mpito ya Somyalia ,amearifu kwamba uchunguzi umeanzishwa kujua chanzo cha ajali hiyo.

Mohamed Mahmoud Guled ameuambia mkutano wa waandishi habari kwamba kisa hiki kina alama zote za hitilafu ya kiufundi.

Mashahidi ardhini wanadai ndege hiyo ilitunguliwa kwa kombora.