Rais Tayyip Erdogan wa Uturuki yuko ziarani nchini Urusi kuzungumzia masuala ya Syria// Jaroslaw Kaczynski hakuweza kuzuwia kuchaguliwa tena rais wa baraza la Ulaya Donald Tusk// Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari amerejea nyumbani hii leo kutoka Uingereza ambako alikwenda kwa matibabu// Maandalizi kwa ajili ya kikao cha halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) yanaendelea huko mjini Dodoma.