Kiongozi wa SPD Martin Schulz, amesema hatochukua wadhifa wa uwaziri katika serikali mpya ya Ujerumani, kufuatia shinikizo kutoka ndani ya chama // Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linatafakari kuhusu rasimu ya azimio la kusitisha mapigano kwa siku 30 nchini Syria // Jeshi la Misri limetangaza kuanzisha operesheni mpya dhidi ya wapiganaji wa kundi linalojiita Dola la Kiislamu - IS